• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

WORLD VISION YAUNGA MKONO MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA KWA KUGAWA VYANDARUWA 6,160 ITILIMA

Posted on: September 9th, 2020

Na. Haruna Taratibu

Shirika lisilo la Kiserikali la World Vision Tanzania kupitia Mradi wake wa Kanadi wilayani Itilima limeendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya tano za kupambana na kutokomeza Malaria katika jamii ya Wanaitilima Mkoani Simiyu kwa kutoa vyandaruwa kwa watoto 6,160.

Zoezi hilo la utoaji wa vyandaruwa vyenye viuatilifu vinavyodumu muda mrefu lilifanyika kwa watoto wafadhiliwa 3,431 na wasio wafadhiliwa 2,729 kwa ujumla wao wanaishi katika mazingira magumu na hatarishi.

Akiongea katika hafla ya kukabidhi vyandaruwa hivyo Mratibu wa Mradi kutoka World Vision Ndg. Nyamoko George amesema kuwa Shirika hilo katika Miradi yake yote limejikita katika kuhakikisha watoto wanapata ustawi katika Nyanja zote za elimu, Afya, na Usalama na haki zao.

“tunaamini kwa vyandarua hivi , maambukizi ya Malaria yatapungua kama si kuisha kabisa, tukizingatia Mpango Mkakati wa Wizara (NMCP) ni kupunguza kiwango cha maambukizi ya Malaria Kutoka asilimia 7 hadi chini ya asillima moja ifikapo mwaka 2020 na kuitokomeza kabisa malaria ifikapo 2030” alisema Ndg. Nyamoko

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Itilima Dkt. Anold Msiba amesema kuwa Malaria bado ni ugonjwa unaosumbua Wananchi Wilayani Itilima na takwimu zinaonyesha kuwa kiwango cha maambukizi kwa wilaya ni asilima 5.1.

“Hata hivyo Halmashauri imekuwa ikishirikiana na Wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwa pamoja na kuelimisha wananchi kufuata kanuni na njia mbalimbali za kujikinga na Malaria kwa kutumia vyandaruwa vyenye Viuatilifu vya muda mrefu sambamba na upuliziaji viuadudu vya Ki-baiolojia kwenye maeneo yenye mazalia ya mbu na kutoa tiba kinga kwa Mama wajawazito” amesema Dkt. Msiba

Akikabidhi vyandaruwa hivyo kwa walengwa kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima Mhe. Benson Kilangi, Katibu Tawala wa Wilaya Ndg. Filbert Kanyirizu aliwaasa Wazazi na Walezi wa Watoto hao kutumia vyandaruwa hivyo kama ilivyo kusudiwa na kuhakikisha wanawahi haraka katika vituo vya kutolea huduma za Afya pindi wanapo hisi dalili za ugonjwa wa malaria.

Wilaya ya Itilima katika mapambano dhidi ya Malaria imekua ikishirikiana na Wadau mbalimbali wakiongozwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Mpango wa Taifa wa kudhibiti Malaria, World Vision Tanzania, USAID Boresha Afya, AMREF, TMARC, Johns Hoppkins University, PSI na Chama cha Msalaba mwekundu Tanzania (TRCS) wadau hawa kwanamna moja ama nyingine wamehuisha lengo la serikali la kutokomeza Ugonjwa wa Malaria nchini ifikapo mwaka 2030 lenye kaulimbiu ya “ZIRO MALARIA INANZA NA MIMI” .

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa