• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

Posted on: June 26th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Kenani Kihongosi ameshiriki Zoezi kuwaapisha Wajumbe wa BARAZA la ardhi na Nyumba la Wilaya ya Itilima, ikiwa ni Rasmi kwa Baraza hilo kuanza kuhudumia Wananchi wa Wilaya ya Itilima.

Aidha wajumbe hao walioapishwa watakuwa na Jukumu la kuhudhuria Vikao  vya Baraza na kusikiliza kesi na kutoa Maoni Yao kwa Maadhishi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Kenani Kihongosi akitoa Rai na kuwataka wajumbe wa Baraza la Ardhi kuwa waadilifu


Aidha Mhe.alsema "Wajumbe Mnapaswa kuzingatia  Miiko ya Wajumbe wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya kama ilivoainishwa na Sheria ya Mahakama ya Ardhi Na 2 ya Mwaka 2002 na Kanuni ya 172 ya Mwaka 2003 na Mwongozo wa Sheria za Mahakama ya Ardhi ya Mwaka 2005"

Mhe. KIHONGOSI aliainisha Sheria hizo ambazo ni
1. Kuwa Mtu mwenye kujiheshimu
2. Kuishia na uonekane ni Mtu usiye na upendeleowa aina yoyote.
3.  Usishiriki kutoa Maamuzi au Kusikiliza kesi yoyote itakavyo kuhusu wewe Binafsi au Mtu yoyote kutoka katika Familia Yako.
4. Ujue mipaka ya Kazi Yako na kwa namna yoyote usijaribu au kuonyesha kuwa wewe unafanya Kazi za Mwenyekiti.
5. Wakati wote uwe msiri kuhusiana na kesi ambazo bodo kutolewa uamuzi, hairusiwi kusema nje ya Baraza kitu chochote kinacho hisu undani wa kesi ambayo haija hamuliwa.
6. Haurusiwa kuwa na Urafiki wa Upande wowote na upande wowote katika kesi inayo endelea kusikilizwa
7. Hairusiwi kuwa wakili wa Upande wowote katika kesi, hairusiwi kutoa Ushauri au kuwaandikia wadaiwa kitu chochote katika kesi.
8. Kujiepusha na kuzungumza au kufanya Mawasiliano yoyote na wadaiwa katika eneo la Baraza na kwa Hali yoyote hairusiwi kutoka nje ya Jengo la Baraza kwenda kuzungumza na Wadaiwa au jamaa zake kabla au baada ya Saa za Kazi.
9. Kuwahi na kuhudhuria katika Vikao kama itakavyo kuwa imepangwa na Mwenyekiti na usikose kuhudhuria mfululizo wa Vikao kwa. Kipindi kisicho dhidi Mwezi Mmoja bila sababu ya kuridhisha.
10. Usimshawishi Mwenyekiti wa Baraza ili akupangie uketi kwenye kesi Fulani
11. Baada ya Kukamilika kusikilizwa kwa kesi Fulani mjumbe utatoa Maoni Yako kwa Maadhishi bila kuchelewa.

12. Usipokee au kuomba zawadi kama hongo na takrima kutoka upande wowote wa wadaiwa.

Wajumbe wa Baraza la Ardhi wakisaini HATI ya  Kiapo baada baada ya Kila kiapo


Mhe. KIHONGOSI alihitimisha kwa kuwatakiwa Wajumbe hao utekelezaji mwema wa majukumu Yao mapya kwa wanaitilima.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Itilima Mhe. Anna Gidarya alisema
"Sasa tuna Imani kesi hizi za Ardhi zinaenda kupata utatuzi"

Aidha Mhe. Gidarya alimuomba Mkuu wa Mkoa wa Simiyu  kufikisha salamu za Wanaitilima kwa Mhe. RAIS, Dkt. Samia Suluhu Hassan Kwa kutusogezea Huduma hii kwa Wananchi na Mimi kama Kiongozi wao naahidi  tutalilea Baraza ili lihidumia Wananchi kwa Weledi, ili kuendelea kuunga Mkono Jitihada za Mhe. RAIS za kusogeza Huduma Muhimu kwa Wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Itilima Mhe. Anna Gidarya akielezea Changamoto waliyo ipitia wanaitili huku wakisafiri kwenda kutafuta huduma  ya Baraza Wilaya ya Maswa


Awali, Kaimu Katibu Tawala ambaye ni Afisa Sheria wa MKOA wa Simiyu Bi. Mwanahamisi Kawega akiwasilisha Taarifa Kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa yakwambwa.

Tangu uanzishwe Mkoa wa Simiyu kumekuwa na Baraza la Ardhi na Nyumba katika Wilaya ya Maswa na limekua likihudumia Mkoa mzima wa Simiyu.


"Lakini kwa idhini ya Mhe. Rais. Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mwaka Jana tulizindua Baraza kingine katika Wilaya ya Busega na Sasa tunawaapisha Wajumbe wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Itilima lakini Mpango iliyopo ni Kila Wilaya ifikiwe na Huduma ya Mabaraza ya Ardhi.

Kwa upande wa Kamishna wa Ardhi Mkoa Alimshukuru Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa Kuwaapisha Wajumbe wa Baraza la Ardhi la Itilima, na Kuushukuru Uongozi wa Wilaya ya Itilima Kwa kulipatia Baraza Jengo litakalo tumika kama Ofisi ya kutekeleza Majukumu ya Mbalimbali ya Baraza.  


 










Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa