• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

WAZIRI MPINA AAHIDI YAFUATAYO ITILIMA;

Posted on: February 12th, 2020


  • KULETA SIKU YA UHIMILISHAJI KITAIFA WILAYANI ITILIMA

  • UJENZI WA MAJOSHO MATATU KATIKA BAJETI IJAYO YA WIZARA YA MIFUGO

  • VIJIJI VILIVYO KANDOKANDO MWA HIFADHI KUCHUNGA NDANI YA MITA 500

Waziri wa mifugo na uvuvi Mhe. Luhaga Mpina ameahadi kuleta kampeni ya kitaifa ya uhimilishaji wa mbegu bora ya Mifugo wilayani Itilima ambapo huduma hiyo itatolewa bure kwa ng’ombe 1,000/ na baada ya hapo zoezi hili litafanyika kwa Tsh. 10,000/ kwa ng’ombe badala ya Tsh. 30,000/ bei ya awali.

Akiongea na Wafugaji Wilayani Itilima Mhe. Mpina alisema“Serikali ya awamu ya tano inayo ongozwa na Mhe. Rais John Pombe Magufuli imekusudia kuimarisha sekta ya mifugo ili kwenda sambamba na uchumi wa viwanda na ndiyo maana Serikali hii imejenga machinjio bora na za kisasa katika baadhi ya mikoa nchini Ikiwemo machinjio ya Dar es Salaam yenye uwezo wa kuchinja Ng’ombe 1000 kwa siku na Viwanda vya kuchakata malighafi mbalimbali zitokanazo na Mifugo”

Aidha Mhe. Mpina alisema ya kwamba uwepo wa machinjio hizi utaenda sambamba na mabadiliko makubwa katika sekta nzima ya mifugo ikiwemo uboreshaji wa Miundombinu yote inayo hitajika majosho, upatikanaji wa madawa sahihi ya Mifugo, pamoja na kufanya uhimilishaji wa mbegu bora ili kuwa na mifugo yenye afya na ya kisasa.

Mhe. Mpina aliongeza ya kuwa “Mhe. Rais Magufuli kwa kutambua umuhimu wa sekta ya Mifugo amefuta pendekezo la kuhamisha vijiji 920 vya Wafugaji vilivyopo ndani ya mita 500, kutoka eneo la mpaka wa hifadhi mbalimbali nchini na kipindi cha kiangazi eneo hilo la mita 500 litatumika kwa malisho ya mifugo, kwa upande wa Itilima, vijiji vilivyopo katika orodha hiyo ni Mwaswale, ng’walali, Nyantugutu, Mwamakili, Mbogo, Pijulu, Shishani , Longalombogo na Ndingho ”.

Sanjari na hayo, Mhe. Mpina alisisitiza kwa wafugaji kuhakikisha wanaogesha mifugo yao kila inapo hitajika “ kwani magonjwa mengi ya mifugo yanatokana na kupe, tukijikita kikamilifu katika uogeshaji tutaweza kuokoa mifugo mingi sana na katika kufanikisha zoezi hili Serikali kupitia ruzuku ya dawa ya kuogeshea mifugo inayo tolewa kila baada ya miezi sita, sasa mfugaji ataogesha Ngo’mbe mmoja kwa Tsh. 50 na mbuzi au kondoo wataoga kwa Tsh. 10” alisema Mhe. Mpina.

Ili kufikia malengo hayo Waziri. Mpina alimuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima Bi. Elizabeth M. Gumbo kuhakikisha ukarabati wa majosho ambayo hayatoi huduma za uogeshaji unafanyika na Kupitia Wizara ya Mifugo watakarabati Majosho matatu.

Baada ya kuuliza changamoto zinazo wakabili Wafugaji, lilijitokeza suala la wafugaji walio taifishiwa mifugo yao (ng’ombe) 336 na Mamlaka ya Hifadhi ya Poli la Akiba la Maswa mwaka 2017, lililo wasilishwa na Makamu Mwenyekiti wa jumuhiya ya Wafugaji Wilayani Itilima Ndg. John Ludeya na kutiliwa mkazo na Ndg. Alex Mageme Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Itilima.

Bw. Ludeya alisema yakwamba mifugo 336 iliyo taifishwa ilikutwa ikichunga katika maeneo ya kandokando mwa Hifadhi hiyo, lakini mapema mwaka huu (2020) wafugaji hao kwa idhini ya mahama iliamuliwa warudishiwe Mifugo yao na mamlaka ya Poli hilo lakini cha kusikitisha wamerudisha ng’ombe 47 na ndama 4 kwa maelezo ya kwamba ng’ombe wengine walikufa.

Kufuatia maelezo hayo Mhe. Waziri Mpina alimuagiza Mganga Mkuu wa Wizara na Mwanasheria wa Wizara hiyo kubaki Itilima na kumuagiza Mkuu wa Wilaya ya Itilima Mhe. Benson Kilangi kumwita Meneja wa Poli la akiba la Maswa, Mwenyekiti wa Wafugaji pamoja na wafugaji wanne waliyo taifishiwa ng’ombe zao na nyaraka zao zote, kukutana kesho chini ya uwenyekiti Mhe. Kilangi kujadili suala hili kwa kuzingatia sheria za mifugo na Maamuzi yaliyo tolewa na Mahakama na Waziri apewe mrejesho ili ajue pakuanzia na haki iweze kupatikana

Sekta ya mifugo nimiongoni mwa sekta muhimu sana kuelekea uchumi wa viwanda lakini changamoto lukuki zinazo ikabili sekta hii, ikiwemo magonjwa, uhaba wa malisho, migogoro ya Wakulima na wafugaji, ufugaji usiyo zingatia utaalamu na uwekezaji wa viwanda vya kuchakata mazao ya mifugo, imepelekea sekta hii kudumaa na kuendeshwa bila tija na wafugaji wenyewe kuishi katika maisha ya umaskini mkubwa.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa