• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

WANAO HUJUMU MIRADI YA MAJI ITILIMA WAONYWA.

Posted on: November 2nd, 2022

Uongozi wa Wilaya ya Itilima  umewaonya baadhi ya watu wanahujumu  miundombinu ya maji iliyojengwa na wadau wa maendeleo Wilayani humo kwa ajili ya kusogeza huduma hiyo muhimu kwa jamii.

Aidha imebainika kuwa licha ya wadau wa maendeleo wilayani humo kujitahidi kutumia gharama kubwa ili kuwasogezea wananchi huduma muhimu kwa lengo la kuwasaidia kuondokana na adha mbalimbali zinazowakabili baadhi ya watu wamekosa uaminifu na kuamua kufanya uharibifu.

Onyo hilo limetolewa na Mkuu  wa Wilaya ya Itilima Mhe. Faidha Salim wakati akikagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Shirika lisilo la Serikali la World Vision na kusema kuwa Mamlaka haitosita kuchukua hatua dhidi ya watu/mtu yeyote atakayebainika kufanya uharibifu kwenye mradi wowote wa maendeleo.

Mhe. Faidha amesema kuwa kufanya hivyo ni kuwakatisha tamaa wadau waliojitoa kwa ajili ya maendeleo na kusaidia wananchi kuondokana na changamoto zinazowakabili, alisisitiza kuwa  hatamvumilia yeyote atakaye patikana kuhujumu miradi.

Ameongeza kuwa kila mmoja anao wajibu wa kulinda na kuitunza miradi ili isiharibiwe kwa ajili ya manufaa ya kizazi hiki na kijacho huku akikisitiza utoaji taarifa dhidi ya inayoharibiwa kwa ajili ya manufaa ya vizazi vyao na vijavyo.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa kijiji cha Kilugala Lulu Mang'ombe ameeleza kuwa kabla ya kupata mradi huo walikuwa wanalazimika kutembea umbali mrefu wa Kilomita 5 kwenda kutafuta maji ambapo yalikuwa ya kwa shida.

Akieleza juu ya uharibifu wa mradi  wa maji Mang'ombe amekiri kufanyika kwa uhujumu katika mradi na hii ni kutokona na kusitishwa kuchota maji bure na kulazimika kulipia jambo lililopelekea sintofahamu kwao na kusababisha tatizo hilo na hii ni kwa sababu  ya ukosefu wa  elimu ya kutosha juu ya mradi huo ambapo kwa sasa imeanza kutolewa.

Kwa upande wa Mratibu wa mradi wa Kanadi na Luguru Nyamoko amesema kuwa mradi huo wa Kilugala  umegharimu kiasi cha Tshs. Milioni 460/ na unauwezo wakuhudumia wakazi zaidi ya 8, 000 pamoja na vijiji 3.

Aidha Mratibu huyo aliainisha Miradi mingine iliyofadhiliwa na Shirika hilo ni pamoja na ujenzi wa vyoo matundu 8 katika shule ya Msingi Chinamili uliogharimu kiasi cha shilingi milioni 42 ambapo wanafunzi zaidi ya 1000 wananufaika na mradi huo.

Ujenzi wa Zahanati ya Ikungulipu iliyopo katika kata ya Luguru umegharimu kiasi cha shilingi milioni 142 na unahudumia wagonjwa 80 kwa siku.

World Vision inatekelezaji wa Mradi wa Maji katika Kijiji cha Nangale kilichopo katika Kata ya Ndoleleji Mradi huo Unajumuisha Tenki lenye ujazo wa Lita elfu 50, na vituo vya kuchotea maji vitano na nyumba ya Mitambo kwa ujumla mradi  umegharimu kiasi Cha Tshs.  Milioni 217/- na utahudumia wakazi zaidi 2000.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa