• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

SIMIYU INAVYO JIPAMBANUA KUELEKEA MABADILIKO YA KWELI KUPITIA SEKTA YA ELIMU

Posted on: October 30th, 2019


Naibu waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu anaye shughulikia Watu wenye Ulemavu Stella Ikupa amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka kwa jitihada zake za Makusudi za kunyanyua Maendeleo ya Mkoa wa Simiyu hususani katika sekta ya Elimu.


Akizungumza katika kilele cha ufungaji wa Makambi maalimu ya kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne Mhe. Ikupa alisema


"Nampongeza Mkuu wa Mkoa kwa ubunifu huu wa kuandaa Makambi haya naamini wanafunzi mmejifunza mambo mengi na mtafanya vizuri katika mtihani wenu na ningeshauri viongozi wengine waige jambo hili"


Aidha Mhe. Ikupa alisema serikali inaendelea kuboresha sekta ya Elimu nchini kwa kuongeza bajeti katika Shule, kujenga madarasa na itaendelea kutatua changamoto za Walimu katika Mkoa huu na Nchi kwa ujumla.


Akiongea na hadhara hiyo Mhe. Mtaka alisema

" kwa uwekezaji uliyofanyika kwa watoto hawa na walimu mahili kwa kushirikiana na viongozi wazazi na wadau mbalimbali naamini watafanya vizuri Mitihani yao ambayo itaanza hapo Novemba 4, mwaka huu"


Aidha Mhe. Mtaka alisema Kama Mkoa wataendelea kutoa motisha kwa Walimu na watoto watakao Fanya vizuri katika matokeo ya kitaifa.


 Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abas alisema kuwa kupitia Kambi hii anamatumaini ya kuwa kutapatikana Viongozi mahiri na kuahidi kuendelea kuunga mkono jitihada za wanafunzi kutimiza ndoto zao.


Kwa niaba ya Chama cha Walimu Tanzania CWT katibu Mkuu wa chama hicho Ndg. Deus Seif  aliunga mkono jitihada za Mkuu wa Mkoa katika maendeleo ya Elimu kwa kutoa Mifuko 500 ya Saruji na kuwashukuru Walimu kwa kujitoa kwao na ushirikiano waliyo uonyesha.


Akitoa maelezo ya kina kuhusiana na Kambi hii  Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu Ndg. Elnest Hinju alisema


" Kambi  ilikuwa na jumla ya wanafunzi 1512 ambao walipata fursa ya kukaa kambini kwa takribani miezi miwili na kufundishwa na walimu mahili, kusoma kwa bidii pamoja na kujifuza masuala mbali mbali ya kijamii"


Akiwakilisha wanafunzi waliyo hudhuria katika Kambi hiyo Mwanafunzi Magreth Sonda kutoka shule ya sekondari Simiyu alisema


"Kupitia Kambi hii tumejifunza mambo mengi kwa Walimu wetu ikiwemo mbinu mbali mbali za ujibuji wa maswali na kwa mitihani tuliyofanya ufaulu wetu umekuwa ukipanda na naamini tutafanya vizuri mitihani yetu ya mwisho.


Tangu Kambi hii zianze rasmi mwaka 2016 zimesaidia kuongeza kiwango cha ufaulu katika matokeo ya kidato cha nne  ambapo mwaka 2017 ufaulu ulikuwa 70.68% na mwaka 2018 ufaulu ulikuwa  86.46% na Simiyu kushika nafasi ya 9 kitaifa.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa