• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

MJUMBE WA BARAZA LA WAFANYAKAZI LAZIMA AWE NA UWEZO WA KUCHUNGUZA CHANZO CHA TATIZO BAINA YA TAASISI NA WAFANYAKAZI ANAO WAWAKILISHA: LUGINGA

Posted on: January 29th, 2020


MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFANYAKAZI LA HALMASHAURI (W) ITILIMA BI. ELIZABETH GUMBO AKIPOKEA MKATABA  KUTOKA KWA AFISA KAZI KUTOKA OFISI YA WAZIRI MKUU SERA,URATIBU BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU KANDA YA MWANZA NDG. GOODLUCKY LUGINGA, KULIA NI MAKATIBU WA BARAZA.

Wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima wameaswa kufanya kazi kwa kujituma na kuepuka vitendo vya ulevi wakati saa za kazi na ufanyakazi kwa mazoea ili kuwa mfano wa kuigwa katika jamii inayowazunguka

Akiongea na Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi la Halmashauri ya Wilaya ya Itilima Afisa Kazi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu kanda ya Mwanza Ndg. Goodlucky Luginga alisema

“sisi kama wafanyakazi tunapaswa kufanya kazi kwa kujituma muda wote na vitendo vya ulevi wakati wa kazi ni mwiko na ni kosa la kuachishwa kazi hivyo aliwaomba wajumbe wa Baraza wakawapatie taarifa hiyo Watumishi wenzao wanao wawakilisha”

Akiainisha majukumu ya Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi Ndg. Luginga alisema yakuwa Mjumbe wa Baraza hilo lazima awe na uwezo wa kuchanganua mambo kwa ufasaha, kuchunguza chanzo cha tatizo kati ya Taasisi na Wafanyakazi anao wawakilisha na alisisitiza kwa kuainisha majukumu ya Baraza la Wafanyakazi ambayo ni kupanga mipango ya Halmashauri, kuimarisha mipango hiyo na kuwashawishi na kuwahimiza Wafanyakazi kufanya kazi, Kupokea mapendekezo ya mapato na matumizi ya Halmashauri”

Sanjari na hayo , Afisa kazi huyo aliwaomba Wajumbe kabla ya kuhudhuria Baraza wapite kwa wajumbe wanao wawakilisha ili kuweza kupata maoni yao, pia kuwapatia mrejesho wa Baraza ili waweze kutathimini kiasi cha maoni yaliyotekelezwa na ambayo hayajatekelezwa.

Baraza la Wafanyakazi lilikuwa chini ya Uwenyekiti wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima Bi. Elizabeth Gumbo ambaye kabla aliongoza uundwaji upya wa Baraza kwa kuwasililisha majina ya wagombea kwa nafasi ya Katibu na Katibu msaidizi ambapo wajumbe walimchagua BI. Joyce A. Mhando Ambaye ni Afisa Utumishi kwa nafasi ya Ukatibu wa Baraza kwa kura 25 na Athony P. Masilu (afisa Mipango Msaidizi) kwa nafasi ya Ukatibu Msaidizi wa Baraza kwa kura 24.

Wakijadili Mapendekezo ya Rasimu ya Bajeti ya Mapato na Matumizi maeneo yasiyopata ruzuku na yanayo pata ruzuku mwaka 2020/2021 na Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2020/2021 hadi 2022/2023 wajumbe wa Baraza la wafanyakazi waliibuka na hoja zifuatazo

Akihoji kuhusiana na idadi ya maduka yaliyo orodheshwa kama chanzo Katibu wa CWT wilaya ya Itilima Ndg. Njile A. Lufasinza alihoji ya kuwa idadi ya maduka ni ndogo na kuomba idara husika ifanye utafiti ili kupata idadi kamili ya maduka ya nguo katika Halmashauri

Akijibu hoja hiyo Mkuu wa idara ya Mapato Ndg. Sile Sefu alisema ya kuwa idadi hiyo inatokana na idadi ya maduka yanayostahili kulipa leseni, kuhusiana na uanzishaji wa kituo cha Magari ya abiria katika Kata ya Luguru, Ndg Sefu alijibu ya kuwa.

“Tumekusudia kuanzisha kituo cha Magari ya abiria katika Kata Mwamapalala, ndiyo maana Chanzo hiki tumekiweka kwenye Rasimu yetu ya Bajeti kama chanzo cha Mapato.

WAJUMBE WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WAKISIKILIZA KWA MAKINI MAELEZO YA MWENYEKITI WA BARAZA BI. ELIZABETH GUMBO (HAYUPO KATIKA PICHA

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa