• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

MIRADI YENYE FEDHA ITEKELEZWE KWA HARAKA: DC ITILIMA

Posted on: November 27th, 2018


Madiwani wa Itilima wakiwa katika kikao cha kwanza kwa cha Baraza kwa mwaka mpya fedha 2018/2019


Mkuu wa wilaya ya Itilima Mhe. Benson Kilangi ameitaka ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Itilima kukamilisha kwa wakati Miradi yote ya Maendeleo iliyotengewa  fedha.

Akitoa Taarifa  za Serikali kwenye Kikao cha Baraza Madiwani la kwanza kwa mwaka mpya wa fedha 2018/2019, Mhe. Kilangi alisema  “utekerezaji wetu wa Miradi ni mzuri na umeendelea kutujengea taswira nzuri mbele ya viongozi wetu wa Mkoa na Kitaifa, tusije kulegalega na kuchafua taswira ambayo imetughalimu kuijenga, ninaomba Miradi yote yenye fedha ikamilike kwa wakati”.

Vile vile  Mhe. Kilangi alizungumzia  suala la ukusanyaji wa Mapato na kuitaka ofisi ya Mkurugenzi kujiwekea Malengo ya Jinsi gani Halmashauri itafikia asilimia 81 ya makusanyo iliyowekwa kwa kila Halmashauri “ Mkurugenzi katika hili kaa na timu yako ya uongozi (C.M.T) muangalie ni jinsigani mtaunganisha nguvu kazi na kuyafikia malengo haya” alisema Mhe. Kilangi.

Sanjari na hayo Mhe. Mkuu wa Wilaya  alizungumzia suala la Pamba hususani ugawaji wa Mbegu za pamba kwa wakulima. Zoezi ambalo limekamilika  na aliwataka viongozi kushiriki kikamilifu kusimamia zao hili ambalo ndiyo zao Kuu la Biashara kwa Itilima.

Akimpongeza  Mkuu wa Wilaya kwa kile alichoeleza kuhusiana na Pamba Diwani wa Kata ya Kinang’weli Mhe. Scania J. Luyombya alisema

 ”nikupongeze Mhe Dc kwani ni Viongozi wachache sana huonekana wakati wa maandalizi ya mwanzo ya kuwaandaa wananchi kwa ajili ya msimu Mpya wa kilimo cha pamba, wengi wao huonekana wakati wa mavuno”

Akitoa ufafanuzi jinsi ya kuepukana na utegemezi wa zao moja tu, Mhe Scania alisema “ Mhe. Mkuu wa Wilaya, wilaya yetu tumepata bahati ya kuwa na mazao mchanganyiko mengi sana, tumeshindwa kuyadhibiti tu na kuyafanya kuwa mapato na kupitia udhaifu huu, wajanja wanayavusha mazao yetu bila kutozwa ushuru na kwenda kuzinufaisha wilaya za Jirani.Tukijizatiti katika usimamizi tutaondokana na utegemezi wa pamba kama zao pekee la kiuchumi wilayani Itilima”

Kwa upande wa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima Ndg. Kelisa Wambura alielezea shughuli zinazo tekelezwa na Ofisi ya Mkurugenzi kwa sasa ni ujenzi  wa ofisi ya Mkurugenzi awamu ya pili ambao  unaendelea vizuri.

Aidha Kaimu Mkurugenzi huyo alisema “ kwa sasa tupo katika maandalizi ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya inayo tarajiwa kujengwa katika Kijiji cha Nguno kilichopo katika kata ya Lagangabilili na baadhi ya vifaa vya ujenzi kama  mawe na Mchanga vimeshaanza kupelekwa katika eneo la ujenzi.

Vile vile Ndg. Wambura alizungumzia  maandalizi ya kuwapokea  Wanafunzi wa Darasa la kwanza na Kidato cha Kwanza ambapo alisema kunauhitaji wa Vyumba 40 vya madarasa kwa shule za sekondari na vyumba 1635 kwa shule za Msingi zilizopo wilayani Itilima.

Kikao cha kwanza cha Baraza la Madiwani kwa mwaka huu mpya wa fedha 2018/2019 kilihitimishwa kwa kuhazimia yafuatayo ikiwemo utekelezaji wa miradi yote yenye fedha kwa wakati, ziara za kamati mbalimbali zifanyika kwa wakati sahihi na ukamilishaji wa miundombinu katika gulio la Lagangabilili ndani ya wiki Mbili  


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa