• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

KAMATI YA FEDHA YAKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI 1.89 KATIKA KATA NNE ZA TARAFA YA KANADI

Posted on: October 21st, 2021

Na. harunataratibu82@gmail.com

Kamati ya Fedha na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Itilima yafanya ziara na kukagua utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo yenye thamani ya Sh. Bilioni 1.89. katika Kata ya Mhunze, Migato, Ikindilo na Lagangabilili.

Ziara hiyo ilikagua   Miradi ya Elimu yenye thamani ya Sh. Milioni 240/= ikihusisha Miradi ya ujenzi wa vyumba vinne vya Madarasa na Ofisi katika Shule ya Msingi Madilana na Shishani vyenye thamani ya Sh. Milioni 80/= .

Aidha kamati ilikagua Mradi wa ujenzi wa  vyumba vinne vya Madarasa na Ofisi mbili katika Shule ya Sekondari ya Chinamili vyenye thamani ya Sh. Milioni 80/=, pamoja na Ujenzi wa Mradi wa Bweni la watoto wa kike katika Shule ya Msingi Lagangabili uliyo pata ufadhili wa kiasi Cha pesa Sh. Milioni 75/= ujenzi ukiwa katika hatua za awali.

Hata hivyo katika Miradi hiyo ya Elimu, wasimamizi wa Mradi wa Shule ya Msingi Shishani na Shule ya Sekondari Chinamili walitakiwa kuhakikisha wanamaliza Miradi hiyo kwa haraka kutokana kuwa nje ya muda wa kukabidhi

"Hakikisheni mnamaliza miradi hii haraka sababu mpo nje ya muda wa kukabidhi" Mhe. Daudi Nyalamu Mwenyekiti Wa Halmashauri.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Itilima Bi. Elizabeth Gumbo aliwataka wasimamizi wa Mradi wa Shishani na Chinamili kuongeza Mafundi ili kukamilisha Mradi huo kwa haraka.

Katika miradi ya Afya, Kamati ilitembelea  mradi wa ujenzi wa Kituo Cha Afya Cha Kanadi ambapo hivi karibu  Mradi huo ulipata fedha kiasi cha Sh. Milioni 250/ ujenzi ukiwa katika hatua za awali huku Mhe. Nyalamu aliwataka Wananchi wa Kata ya Migato kuchangia nguvu Kazi na kuleta Mchanga, Mawe na Kokoto.

Aidha Mhe. Nyalamu aliwapa muda wa siku saba wa kuonyesha ushirikiano Wananchi wa Kata ya Migato kabla ya kuamua kuhamisha Mradi huo na kupeleka sehemu nyingine.

Wakiwa katika Hospitali ya Wilaya, kamati iliridhishwa na utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa Wodi tatu zilizo tengewa kiasi Cha Sh. Milioni 500, ikihusisha Wodi ya watoto, Wodi ya Wanawake na Wodi ya Wanaume, huku  Wodi ya watoto na Wanaume ikiwa katika hatua za Umaliziaji.

Kamati ilipata fursa ya kutembelea Mradi wa ujenzi wa Ghala la kuhifadhia Chakula, wenye gharama zaidi ya Sh. Milioni 900/ uliyofadhiliwa na Serikali kupitia Wizara ya Kilimo na Chakula na kutekelezwa na kampuni ya ujenzi ya Nice (Nice Engineering & Construction Co.) na utahusisha  Ujenzi wa Ofisi na Maabara, ujenzi wa Ghala, ujenzi wa eneo la kukaushia Mazao,Vyoo na uzio.

Wilaya ya Itilima sasa ipo mbioni kuondoka na neno "Wilaya changa" ndani ya kipindi kifupi kijacho kwani huduma zote muhimu zitapatikana ndani ya Wilaya,  na hii ni kutokana na miradi kikubwa  Inayo tekelezwa na itakayo enda kutekelezwa muda si mrefu. 

 Tunakila sababu ya kusema ahsante Serikali ya Awamu ya Sita chini Mama Samia Suluhu Hasani kwa kuamua kutatua  changamoto za huduma stahiki kwa Wananchi wa Itilima na Wanaitilima tunasema Ahsante sana Mama.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa