• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

ITILIMA YAPONGEZWA KUTAMBUA MCHANGO WA WALIMU, VONGOZI, WADAU KATIKA KUKUZA ELIMU

Posted on: March 11th, 2022

Na. harunataratibu82@gmail.com

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila akikabidhiwa cheti na Mwenyekiti wa Halmashauri (W) Itilima Mhe. Daud Nyalamu kama ishara ya kutambua jitihada zake katika kisimamia Mkoa kitaaluma


Mkuuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila amewapongeza walimu wa Halmashauri ya Itilima Kwa kuongeza ufaulu katika mitihani ya kitaifa ya kidato cha nne, kidato Cha pili,darasa la saba na la nne.

Mhe. Kafulila alitoa pongezi hizo katika hafla maalumu ya kuwapongeza walimu wa itilima Kwa kuongeza ufaulu kwa asilimia 6(%)  na kuwa na 96% Kwa matokeo ya kitaifa Kwa shule za Sekondari na asilimia 90 Kwa matokeo ya kitaifa Kwa shule za Msingi.

Mhe. Kafulila aliupongeza uongozi wa Wilaya na wadau wa elimu wilayani humo Kwa kuandaa hafla ya kutambua mchango wa Mwalimu na kutoa  motisha  Kwa walimu kwani tukio hili litajenga shauku ya kufanya vizuri zaidi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila akimkabidhi cheti Mkuu wa Wilaya ya Itilima Mhe. Faidha S.Salim kama ishara ya kutambua jitihada zake katika kisimamia Elimu


" kuongeza ufaulu Kwa asilimia sita na kuwa na ufaulu wa asilimia 96 (%) Kwa Sekondari  na asilimia 90 Kwa Elimu Msingi Kwa Itilima na wilaya zingine ndiyo kumeufanya Mkoa wa simiyu kushika nafasi ya tatu kitaifa Kwa matokeo ya 2020 - 2021

Aidha Mhe. Kafulila alisema kuna kila sababu ya kuwapongeza walimu wetu kwa matokeo haya Itilima na Wilaya zingine zimeufanya Mkoa kushika nafasi ya tatu kitaifa na hii ni hatua kubwa kwa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila akimkabidhi cheti Mwenyekiti wa Halmashauri (W) Itilima Mhe. Daudi Nyalamu kama ishara ya kutambua jitihada zake katika kisimamia taaluma


"Unaposhika nafasi ya tatu kitaifa sisuala dogo ukizingatia changamoto tulizonazo kama Mkoa na maeneo yetu Kwa asilimia zaidi ya 90 ni Vijiji na miundombinu yetu ukilinganisha na wengine, Kwa kweli tunakila sababu ya kuwapongeza Walimu wetu  kazi nzuri wanayofanya.


Mhe. Kafulila alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mama Samia Suluhu Hassan Kwa kiasi kikubwa kutachochea hali ya kufanya vizuri katika elimu Kwa kutuletea Fedha kiasi cha Sh. Bilioni 7.6 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya Madarasa 380.

"Kwa uwekezaji huu wa Mama katika elimu hatutaki kuona upuuziaji wa elimu na naiagiza kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya  kufuatilia utoro rejareja  wa wanafunzi na wazazi wanao waozesha wanafunzi"  
Mhe. Kafulila aliagiza

Kwa upande wa Mkuu wa ya Itilima Mhe. Faidha S. Salim alielezea namna wilaya ilivyo jipanga katika kutatua changamoto zinazo ikabili sekta ya elimu na kuahidi kuandaa Harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya madarasa na nyumba za walimu.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. David Kafulila akimkabidhi cheti Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri (W) Itilima Bi. Elizabeth Gumbo kama ishara ya kutambua jitihada zake katika kisimamia Idara ya Elimu


Akiwasilisha taarifa yautekelezaji Kwa sekta ya elimu, Mkurugezi mtendaji Bi. Elizabeth Gumbo alisema ya kwamba kama Halmashauri wameshaanza kutatua baadhi ya changamoto zinazo ikabili sekta ya elimu Kwa kutenga fedha kutoka katika mapato ya ndani na kizielekeza katika ujenzi wa madarasa.

Katika hafla hiyo Mkuu wa Mkoa aliwatunuku vyeti na Pesa kwa walimu waliyo fanya vizuri, wadau wakubwa wa elimu wakiongozwa na Mzee Katani Ndabagija na Viongozi wa Wilaya wakiongozwa na Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Itilima na mwenyekiti wa Halmashauri ya Itilima alimkabidhi Mhe. Kafulila Cheti kama ishara ya kutambua jitihada za Mkuu wa Mkoa.




Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI YAITENGEA ITILIMA BILIONI 2.37 KUTEGENEZA KM. 238.88 ZA BARABARA NA KM.1 YA LAMI MAKAO MAKUU YA WILAYA

    February 18, 2023
  • NAIBU WAZIRI OR - TAMISEMI ARIDHISHWA UTEKELEZAJI MIRADI YA AFYA ITILIMA

    January 17, 2023
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIO CHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA ITILIMA

    December 14, 2022
  • ITILIMA YAWEKEWA MALENGO KUZALISHA TANI 130,000 ZA PAMBA MSIMU HUU WA KILIMO

    November 28, 2022
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa