• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

ITILIMA KUJIIMARISHA KIUCHUMI KUPITIA "SAMAKI"

Posted on: August 25th, 2020


Na, Haruna Taratibu

Wajumbe  wa Kikosi kazi ya cha ufuatiliaji wa mapato cha Halmashauri ya Wilaya ya Itilima wakiratibu na kufuatilia zoezi zima la uvunaji wa Samaki katika Bwawa la Sawida.


ITILIMA KUJIIMARISHA KIUCHUMI KUPITIA "SAMAKI"

Halmashauri ya Wilaya ya Itilima imeanza zoezi la uvunaji wa Samaki waliyopandwa katika Mabwawa matatu yaliyopo wilayani humo, huku bwawa la sawida likitoa kilo 944 za Samaki katika uvunaji wa awali.

Akielezea Chanzo hiki cha Mapato Mkuu wa Idara ya Mapato Ndg. Sile Salmin Seif alisema

“Uvunaji huu wa samaki unaelekea kuwa chanzo madhuti cha mapato wilayani Itilima, tumeshavua mara tatu katika bwawa la Sawida na tumepata Zaidi ya kilo 900”

Aidha, ndg. Sile alisema kuna uwezekano wa kupata Zaidi ya Milion 20 kwa bwawa moja na Tuna mabwawa 04 yenye Samaki.

Itilima ilibahatika kupata Vifaranga 32,000 mchanganyiko kutoka Chuo cha Utafiti wa Samaki (TAFILI) cha Nyegezi na kuwapandwa, ambapo katika bwawa la Mwamapalala kulipandwa Vifaranga aina ya Sato 7000, bwawa la Sawida lilipata Vifaranga aina ya Sato 5000, huku Bwawa la Habiya kulipandwa vifaranga aina ya Kambale mumi 20,000.

Akitolea ufafanuzi wa chanzo hiki cha Mapato Mkuu wa Idara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Kiraba Msoke alisema

“kwa jinsi tulivyo anza zoezi hili la uvunaji tunapata imani kuwa tunaweza kuwa na chanzo mbadala cha mapato mbacho itilima inaweza kujivunia hapo siku za usoni”

Aidha Dkt. Msoke alibainisha malengo mahususi ya Mradi huu mbali na Halmashauri, Serikali ya kijiji na Jumuiya za Watumiaji maji kupata mapato yatokamayo na Samaki vilevile Mradi utaimalisha hali ya afya na Lishe kwa wanaitilima.

Kwa lengo la kuufanya Mradi huu unakuwa ndelevu, Dkt Msoke alibainisha kuwa usafi wa mara kwa mara katika mabwawa haya utakuwa unafanyika, vile vile kwa kushirikiana na Watu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii watahakikisha wananchi wanapata elemu ya kutosha ya utunzaji wa vyanzo hivi ikiwa pamoja na kutoa ulinzi kwa maeneo haya dhidi ya vitendo uchungaji wa Mifugo kandokando vyanzo hivi na Uvuvi haramu.

Zoezi la uvunaji wa samaki katika bwawa la Sawida linaendelea na litafanyika mara nne kwa Mwezi na mipango ya kuanza uvunaji katika mabwawa yaliyo salia ya Mwamapalala, Habiya na Mwalushu, ipo katika hatua za mwisho.

Wananchi  wakiwa katika mwalo wa bwawa la sawida  baada ya kununua Samaki

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa