• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

DC ITILIMA AWATAKA VIONGOZI AMCOS KUACHA UBINAFSI

Posted on: November 1st, 2018


MKUU WA Wilaya ya Itilima Mhe. Benson Kilangi awataka viongozi wote wa Vyama vya Msingi (AMCOS) kuhakikisha wanawasaidia Wakulima na si kujielekeza kwenye maslahi binafsi na kumuuacha mkulima akikata tamaa  kujihusisha na zao la pamba.


Akiongea na wadau wa zao la Pamba katika kikao cha maandalizi ya Msimu mpya wa kilimo wilayani Itilima, na mapitio ya changamoto zilizo jitokeza msimu uliyo pita, Mhe. kilangi alisema '' dhamana ya Viongozi wa Amcos ni kuwasaidia wakulina na kuhakikisha zao la pamba linaimarika na si vinginevyo na sitaki kusikia  kiongozi wa Amcos ni Mtuhumiwa, ukishatuhumiwa unatakiwa ujiuzuru''


Kauli hiyo ya Mkuu wa Wilaya imekuja baada ya malalamiko ya Wadau wa zao la Pamba kwa baadhi ya viongozi wa Amcos kutokuwa waaminifu kwa makampuni  na kwa wanachama wao.


Akithibitisha uwepo wa tuhuma dhidi ya Viongozi wa Amcos Mkuu wa Kituo cha Polisi Lagangabilili, OCS Bwire alisema

“tumepokea malalamiko kutoka kwa Wanachama wa Amcos kuwa viongozi wao hususani Makatibu wanatumia pesa za wanachama kienyeji na kusingizia zimepotea, tutafanya uchunguzi tukibaini upotevu ni wa kizembe watawajibika”


Hata hivyo Mhe. Kilangi alitoa agizo kwa kamanda wa Polisi Wilaya (OCD) kuhakikisha anawakamata viongozi wote wa Amcos  waliyo hujumu pesa za Wanachama na Makampuni.


Akiongelea Ukopeshaji wa Mbegu za Pamba kwa wakulima, kwa Msimu mpya wa Kilimo, Mhe. Mkuu wa wilaya alimtaka Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima Ndg. Kelisa Wambula kuhakikisha kupitia Watendaji wa Vijiji wapeleke taarifa ofisi ya Mkuu wa wilaya ya majina yote ya Wakulima waliyo pata mbegu na maeneo yao ya Mashamba.


Agizo hilo la Mkuu wa Wilaya limekuja baada ya Maelezo ya Mkaguzi wa Pamba wilaya Ndg. Said Itaso kulalamikia zoezi la ugawaji wa mbegu za Pamba kwa baadhi ya Maeneo kutokuwa na uaminifu baada ya kugawa kwa kutumia Mzani, viongozi wa Amcos wanatumia Makopo kupimia mbegu hizo.


Aidha Mkaguzi huyo wa Pamba alisema kuna baadhi ya makampuni yamekiuka makubaliano ya kuziwekea Mbegu sumu kali, lakini cha kusikitisha wameweka sumu chache, matokeo ya baadae mbegu zinaweza zisikabiliane na wadudu waharibifu.


Bw. Itaso aliomba elimu iendelee kutolewa kwa Wakulima kusafisha masalia ya pamba

Katika mashamba yao ili kupunguza magonjwa na masalia ya waduu wanao baki katika masalia hayo. Vile vile alitoa elimu ya kuandaa dawa ya kukabiliana na unyaukaji wa majani kwa kuchanganya sabuni ya unga kilo moja na mafuta ya kula lita moja , ukipatikana mchanganyiko wa sabuni na mafuta unachanganywa na lita  150 za maji, mchanganyiko huu unatibu magonjwa yanayo ikabili pamba.


Msimu mpya wa kilimo umeanza na Serikali kupitia Bodi ya pamba wameipatia Wilaya ya Itilima tani 1400 za mbegu ya pamba ili wakulima wakopeshe, ingawa  kuna changamoto ya kuto tosha kwa mbegu hizo. Msimu wa mwaka huu Wilaya ya Itilima iliweza kuvuna Pamba kiasi cha kilo milioni 18 na mwaka jana ilivuna kilo milioni 11.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa