• MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
Itilima District Council
Itilima District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Sisi ni nani?
    • Dira na Dhamira
    • Taarifa ya Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango
      • Afya
      • Mifugo
      • Kilimo
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Sheria
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
    • Muundo
  • Huduma Zetu
    • Vibali vya Ujenzi
    • Leseni za Biashara
    • Umilikaji wa Ardhi
  • Machapisho
    • Sheria
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba Video
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi inayofadhiliwa na Wahisani
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea na Ujenzi
    • Maandiko ya Miradi
  • Zabuni
  • Uwekezaji
  • FFARS LINK

BARAZA LA MADIWANI ITILIMA LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 28.5 KWA MWAKA WA FEDHA 2020/2021

Posted on: February 14th, 2020
  • Wakala wa Barabara Vijijini (TARURA )milioni 623.18
  • Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Bilioni 9.6

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Itilima katika mkutano wake maalumu wa Baraza leo Februari 14, 2020 limejadili na kuidhinisha kwa kauli moja bajeti yake ya Tshs 28, 536,837,339/- kwa mwaka wa fedha 2020/2021

Ambapo Tshs. 1,434,558,653 ni mapato ya ndani ya Halmashauri na Tsh. 1,472,997,839/- ni Mapato ya Ruzuku kutoka Serikali kuu, zikijumuisha Tshs. 21,704,337,000/- kwa ajili ya mishahara na Tshs 3,924,943,847 ni Ruzuku ya Miradi ya Maendeleo.

Akizungumza wakati wakupitisha bajeti hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Daudi Nyalamo amebainisha kuwa

“ili kuwa na dira na kufikia malengo chanya, Halmashauri imeandaa mpango wa mwaka 2020/2021 na Mpango wa muda wa kati 2020/2021-2022/2023 unaolenga kukuza uchumi na kupunguza umaskini na kufikia maendeleo endelevu, ya Kijamii, Kiuchumi na Kimazingira kwa wananchi wake”.

Aidha Mhe. Mwenyekiti aliwaomba Wajumbe kujikita kwenye Mpango huo ambao umeshajadiliwa katika mabaraza mbalimbali ikiwemo Baraza la Wafanyakazi, Kikao cha Ushauri cha Wilaya (DCC) na Kamati ya fedha Utawala na Mipango.

Vipaumbele vya mpango huo uliyo wasilishwa na Afisa Mipango na Ufuatiliaji Ndg. Paulo A. Nyalaja kwa niyaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri (W) Itilima Bi. Elizabeth M. Gumbo Umelenga yafuatayo.

kuboresha na kuimarisha ukusanyaji wa Mapato ya ndani kwa kuongeza mashine za kielektroniki za kukusanyia mapato (POS) ili kudhibiti upotevu wa Mapato, kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ili ikamilike kwa kiwango kinacho kubalika na kuanza kutoa huduma mapema iwezekanavyo, kukamilisha madarasa kwa shule za msingi na Sekondari na kuanza kutumika ili kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia na ukamilishaji wa jengo la utawala.

Miradi ya iliyotengewa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri katika mwaka wa fedha 2020/2021 ni ukamilishaji wa ujenzi wa Zahanati ya Bulolambeshi, Zahanati ya Laini, Zahanati ya Mbogo, Zahanati ya Songambele, Zahanati ya Nkololo na Zahanati ya Kidula kwa Tsh. 213,995,599.98/-

Miradi ya elimu iliyo tengewa Fedha ni Ukamilishaji wa Bweni katika shule ya sekondari Lagangabilili ifikapo juni 2021 kwa Tsh. 45,000,000/- pamoja na ukamilishaji wa ujenzi wa nyumba za walimu 3 katika shule 3 za msingi kwa Tsh. 58,995,746/-

Miradi ya ardhi iliyo tengewa fedha ni pamoja na kulipa fidia na kupima maeneo muhimu kwa ajili ya ujenzi wa Viwanda, Soko na eneo la Maziko.

Diwani wa  Kata Zagayu Mhe. Wiliamu Kuzenza akichangia mada katika kikao cha Baraza maalumu la bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Itilima


Rasimu ya Mapendekezo ya Bajeti ya Wakala wa Barabara Vijijini (TARURA) ya kiasi cha Tsh. Milioni 623.18/ iliyo wasilishwa na Mhandisi Athumani Bakari kwa niyaba ya Meneja wa Tarura Wilaya ya Itilima Mhandisi Chinengo, S.N.Y ililigawa baraza hilo kutokana na hali ya sasa ya uharibifu mkubwa wa mtandao wa Barabara uliyo sababishwa na mvua za vuli kupelekea sehemu kubwa ya Wilaya kutopitika.

Ushauri uliyo tolewa na Baraza kwa Tarura ni kuhakikisha wanakuwa na utaratibu wa kujenga barabara moja na kuikamilisha na kwenda nyingine na kuachana na mfumo wao wasasa wa kutengeneza kila mahali wakijua bajeti yao ni finyu.

Hata hivyo Wakala kwa Itilima umewasilisha maombi ya Fedha za matengenezo kiasi cha Tsh. Milioni 317 kwa Mtendaji Mkuu TARURA ili kukarabati maeneo yaliyo athirika na Mvua za Vuli.

Wahe. Madiwani wakiwa katika kikao cha Baraza maalumu la bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Itilima


Aidha kwa upande wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wamewasilisha mapendekezo ya bajeti ya Maji kwa ujumla kwa mwaka wa fedha 2020/2021 kiasi cha Tsh. Bilioni 9.6 kwa mchanganuo ufuatao

Bajeti ya Miradi inayo endelea itakamilishwa na kuanza kutoa huduma kwa Tsh. Bilioni 3, Miradi ya Ukarabati Wakala uanataraji kutumia Tsh. Milioni 60, Miradi ya upanuzi ili kusogeza huduma kwa Wananchi wakala utatumia Tsh. Bilioni 1.9, Miradi mipya Wakala umepanga kutumia Tsh. Bilioni 4.6, uendeshaji wa ofisi na stahiki za Watumishi Wakala umepanga kutumia Tsh. Milioni 69.

Miradi mipya iliyo pangwa kutekelezwa na Wakala katika bajeti ya 2020/2021 ni Mradi wa Maji Habiya ambao utahusisha vijiji 6 vya Mwazimbi, Bulolambeshi, Bumera, Habiya, Gaswa na Mwandulu na kuhudumia kuhudumia watu 18,361 chanzo chake ikiwa ni bwawa la Habiya, bajeti iliyo kadiliwa kugharamia mradi huu Tsh bilioni 4 na Mradi wa Maji katika kijiji cha Ng’esha ambao utahudumia watu 3,437 na bajeti iliyo kadiriwa kugharamia mradi huu ni Tsh. 650,000,000/-

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA WILAYANI ITILIMA October 30, 2021
  • Tangazo Kwa Watumishi Wapya Wanao endelea kuwasili Wilayani Itilima July 03, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, Wafanyakazi tuungane katika makaribis July 07, 2022
  • "Tutaukaribisha Mwenge wa Uhuru Wilayani Itilima tarehe 9/7/2022 tutaupokea katika Viwanja vya Ushirika, Nyamalapa na mkesha utakuwa katika viwanja vya Halmashuri ya Wilaya ya Itilima Wananchi wote, tuungane katika kuukaribisha Mwenge July 06, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • TUME YA TAIFA YA MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI YAPIMA NA KUKABIZI HATI ZA VIJIJI 25 VILIVYOPO KANDO YA POLI LA AKIBA LA MASWA

    June 30, 2024
  • BARAZA LA ARDHI ITILIMA SASA RASMI BAADA YA KUAPISHWA KWA WAJUMBE WA BARAZA

    June 26, 2024
  • KUNA MAISHA BAADA YA UTUMISHI WA UMMA

    June 20, 2024
  • MWALIMU TIMIZA WAJIBU WAKO WA MSINGI KWA AJILI YA NCHI YAKO, WAZAZI WA TANZANIA NA WATOTO KUZIFIKIA NDOTO ZAO

    June 20, 2024
  • Angalia Zote

Video

BARAZA LA MADIWANI LA MADIWANI LA WILAYAYA ITILIMA LAUFUNGA MWAKA WA FEDHA WA 2020 - 2021
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Business License
  • Procedure for Provision of Buliding Permit
  • https://www.nbs.go.tz/index.php/en/census-surveys/population-and-housing-census/802-sensa-ya-watu-na-makazi-ya-mwaka-2022
  • Land Ownership

Tovuti Mashuhuri

  • Simiyu Regional Commissioner's Office
  • President's Official Website
  • Local Government Revenue Collections Dashboard
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma
  • Salary Slip Self Service
  • FFARS LINK
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    DED - ITILIMA

    Sanduku la Posta: 308 BARIADI

    Simu: +255 28 29 863 29

    Simu: 028 29 863 28

    Barua Pepe: info@itilimadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2016 Kitengo cha TEHAMA. Haki Zote Zimehifadhiwa